0


Tribute: Weah, pictured with the FA Cup in 2000, had a message for his baby son on his shirt but then seemed to let the triumph go to his head (below)Na Osward Ngonyani.


Mara kwa mara nimekuwa nikiandika sana makala za kimataifa kuhusu wachezaji fulani ambao kwa kiasi kikubwa huwa wamefanya makubwa katika mawanda ya soka la kimataifa na hata kuwa gumzo kwa kila aliye mdau wa michezo.

Kwa wiki kadhaa zilizopita nimekuwa nikiwaandika sana akina Messi na Ronaldo, nadhani kwa mtu anayefuatilia mchezo wa soka kwa sasa ni lazima ataniunga mkono kutokana na ukweli kuwa wachezaji hao kwa sasa ‘ndiyo habari ya Mujini’.

Wakati nyakati na enzi zikizidi kwenda kasi, nimejikuta nikikikumbuka kitu fulani cha muhimu sana ambacho kwayo kilinifanya nijilaumu kwa kutokukiandika gazetini kwa muda wote wa uandishi wangu.

 George Weah
Ni kweli tangu nianze kazi ya Uandishi nimewahi kuandika makala nyingi sana kuhusu wachezaji nguli waliowahi kuzikonga nyoyo za mahusuda wengi wa soka la dunia lakini kamwe sikuwahi kuandika makala kuhusu shujaa fulani wa Afrika na dunian kwa ujumla, George Weah.

Weah ambaye ni msomi wa Chuo Kikuu cha Devry cha nchini Amerika kwa siku za karibuni amejikita zaidi katika siasa, alizaliwa miaka 48 iliyopita (Oktoba 1 mwaka 1966) huko Monrovia nchini Liberia.

Mwanandinga huyu ndiye mchezaji wa kwanza kutoka nchi ya Kiafrika kutunukiwa tuzo ya Mwanasoka Bora wa dunia, yaani tuzo ambayo mpaka leo hii hakuna mchezaji yeyote wa kiafrika aliyewahi kuipata.

 On target: Weah only played for a short while at Chelsea but showed his nose for goal
Pamoja na akina Samuel Etoo’, Didier Drogba, Yaya Toure na hata akina Michael Essien kuvuma sana kwa siku za karibuni lakini wote kwa ujumla wao wameshindwa kabisa kuifikia rekodi iliyowekwa na mpambanaji huyu.

Nakumbuka ilikuwa mwezi Desemba, mwaka 1995, ambapo FIFA iliitangazia dunia ya soka kuwa kuwa George Weah amechaguliwa kwa kupigiwa kura kuwa mwanasoka bora wa dunia.

Ni katika mwaka huo, George Weah akawa Mwanasoka Bora wa Ulaya, na haikuishia hapo, akatangazwa pia kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika! Ndani ya mwaka mmoja, akajikusanyia mataji matatu.

 Strength of character: Weah was one of the world's greats at his peak
Hapana shaka haya ni mafanikio yasiyo na mifano katika historia ya soka barani Afrika. Weah ni alama ya soka ya Liberia, aliwahi kutoa misaada kwa timu ya taifa ya Liberia iliyokuwa na hali duni ili iweze kucheza michuano ya kombe la dunia na kombe la mataifa ya Afrika, hii ilichangia kumfanya aheshimiwe zaidi na wananchi wa nchini humo.

Nakumbuka mara baada ya kutunukiwa tuzo hiyo George Weah aliwahi kuibeba timu yake ya Taifa akiwa ndiyo nahodha wa kikosi hicho kwa gharama zake yeye mwenyewe ambapo aliambatana na kikosi hicho kwa ajili ya mchezo wa kimataifa dhidi ya Timu ya Taifa ya Tanzania. 

Watanzania wengi walikuwa wagumu sana kuamini kuwa yeye ndiye haswa alikuwa George Weah. Kila alichokuwa akikifanya pale Sheraton hotel kilionekana kushuhudiwa na watanzania wengi waliokuwa wakimshangaa.

 At home: A few pictures of Weah at his apartment in west London in which he lived while he was at Chelsea
Hata siku ya mechi uwanjani bado macho ya watanzania wengi yalionekana kumshangaa yeye zaidi kuliko kuufuatilia mchezo ule. Walionekana kumpapatikia vya kutosha kutokana na heshima yake wakati huo, heshima ambayo ameendelea kudumu nayo mpaka leo hii kwani hakuna aliyeweza kumfikia.

Takwimu za maendeleo yake katika makuzi ya soka zinaeleza wazi kuwa alianza kusakata kabumbu nchini kwake Liberia kabla ya kuhamia katika klabu ya Monaco ya Ufaransa, na baadae Paris Saint Germain ya nchini Ujerumani.

 Sofa king
Baadaye  mwaka 1995 akaenda kwenye klabu ya AC Milan na ndipo akafikia kilele cha mafanikio yake katika mawanda ya soka. Kwenye uwanja wa nyumbani wa San Siro wa timu ya AC Milan, George Weah alikuwa mfalme aliyependwa sana na wapenzi wa Milan.

Alipewa kila kitu pale Milan, alihusudiwa na kamwe hakubezwa kutoka na rangi yake. Uwezo wake wa hali ya juu katika mchezo wa soka uliwafanya hata wabaguzi wa rangi wa kipindi kile kujikuta wakiwa wapole na hata kuonesha mahaba ya wazi kwa shujaa huyu msomi.

Baadaye, George Weah akaenda kuchezea Chelsea na  kisha Manchester City. Pamoja na mafanikio makubwa katika soka, George Weah hakuwahi kushiriki kucheza fainali za Kombe la Dunia, nadhani hiki ni kitu ambacho kitaendelea kumuumiza nafsi yake milele.

 Weah looking out of his window and on to the Thames
Baada ya umri wake kumtupa kidogo, aliamua kustaafu soka na hata kujikita zaidi katika masuala ya kisiasa ya nchini kwake pasipo kusukumwa na mtu au kikundi chochote cha watu.

Bila shaka alikuwa na shauku kubwa ya kuiona nchi yake ikiongozwa na mtu makini atakayeweza kuifanya itulie na kuondokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe na hata kucheza kombe la dunia.

Mwaka 2005, kwa dhati ya moyo wake akaamua 'kucheza kandanda ya majukwaa ya siasa'. Alishiriki uchaguzi mkuu wa Liberia akigombea nafasi ya Urais wa nchini humo, haikuwa kazi rahisi kama wengi walivyodhani kwani kunako mchezo huo wa siasa alikutana na mabingwa waliobobea katika kuucheza mchezo huo.

 In this photo taken on Saturday, Aug. 9, 2014, Liberian President Ellen Johnson Sirleaf speaks to health workers asking that they should keep working at the ...
Si kwa kuonewa, si kwa kufanyiwa hila, mwanamama Ellen Johnson-Sirleaf alimgaragaza vilivyo mpambanaji huyu maarufu katika mchezo wa soka na hata kumfanya mwanamama huyo kuwa Rais wa kwanza mwanamke katika nchi za bara la Afrika.

Hapana shaka ataendelea kukumbukwa tena na tena kutokana na kile ambacho alikifanya ndani ya dimba. Ataendelea kuwa Shujaa wa miaka yote wa bara la Afrika.

Tamati rasilimali……………………….
(Maoni/Ushauri tuma kwenda namba 0767 57 32 87. Kitabu changu ‘MAGWIJI WA SOKA WALIOWAHI KUITIKISA DUNIA…..’ kipo jikoni kikiendelea kupikwa, Mola akipenda Mwezi Desemba kitakuwa sokoni, NITAWAHABARISHA)

Post a Comment

 
Top