0
Podolski tweets about Berlin Wall after defeat, Arsenal fans totally lose perspective
Mshambuliaji raia wa Ujerumani aneyekipiga kwenye klabu ya arsenal Lukas Podolski amewatibua mashabiki wa klabu hiyo ikwa ni masaa kadha tu mara baada ya timu yao ya washika mitutu wa jiji la London Arsenal kupoteza kwa jumla ya magoli 2:1 dhidi ya klabu ya Swansea hapo jana.

 pod
Wengi wa mashabiki hao wakionekana wakiwa na huzuni kubwa kutokana na matokeo hayo, Lakini Podolski aliandika ujumbe kwenye ukurasa wake maalumu wa tweeter akizungumzia kuanguka kwa ukuta uliokuwa ukiigawanya nchi yake ya Ujerumani katika vipande viwili vya Ujerumani Mashariki na Magharibi pale alipoandika; " Ni miaka 25 sasa  imepita tangu ukuta uliokuwa unaigawanya ujurumani mpaka mwaka 1989 ulipovunjwa  lakini sasa tuko wamoja"

pod
Wakati yeye akisherehekea maadhimisho hayo ya miaka 25 baadhi ya mashabiki wa klabu ya Arsenal wameonekana kukerwa na kitendo hicho hali iliyopelekea kumjibu na kumshauri kujiheshimu kidogo kwani kwa mtazamo wao wanaona kuwa haiwezekani wao wafungwe halafu yeye aandike ujumbe wa namna hiyo kwenye mtanadao huo wa kijamii.
 pod

Post a Comment

 
Top