0
Giroud set for Arsenal comeback against Man United, confirms Wenger
Meneja wa klabu ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger anethibitisha kurejea dimbani kwa mshambuliaji wake raia wa Ufaransa Olivier Giroud kutoka kwenye majeraha yake yaliyokuwa yakimsibu siku ambayo washika mitutu hao watakapokua wakipambana na mashetani wekundu wa Manchester United wiki mbili zijazo.

 Arsenal boss Arsene Wenger says striker Olivier Giroud (left) could return from injury earlier than expected 
Taarifa za awali za kitabibu zilikua zikidai kuwa mshambuliaji huyo atakua nje ya uwanja mpaka mwezi wa January kutokana na maumivu yake ya mguu yaliyokuwa yakimkabili.

Giroud (right) suffered a broken foot against Everton and was expected to be out until early next year
Giroud anaonekana kurejea kwenye hali yake ya kawaida mapema sana kuliko ilivyodhaniwa awali na meneja wa timu hiyo Arsene Wenger amethibitisha kurejea kwa mshambuliaji huyo na amesema kuwa rasmi ataanza mazoezi wiki ijayo.

Wenger also added that Giroud could play alongside striker Danny Welbeck (right) when he returns from injury
Arsenal inatarajiwa kusafiri kwenda kuwavaa vijana machachari wa Swansea mwishoni mwa wiki kabla ya wachezaji kujiunga na timu zao za taifa kwa medani za kimataifa na hivyo kumpa nafasi mshambuliaji huyo kuwa na wiki tatu za kujiweka sawa kabla ya kurejea dimbani kwenye siku ambayo washika mitutu hao watakapokuwa wanawakaribisha Mashetani wekundu wa jiji la Manchester kwenye uwanja wa Emirates hapo November 22.

 Mesut Ozil may have played his last game for Arsenal against Chelsea at Stamford Bridge last Sunday
Halikadharika Wenger amethibitisha maendeleo mazuri ya kiungo Jack Wilshere aliyekuwa anasumbuliwa na matatizo ya virusi na anatarajiwa kuwemo kwenye kikosi kitakacho wavaa Swansea, licha ya kuwa hali ya mlinzi Mfaransa Laurent Koscielny bado haijatengemaa.

 Laurent Koscielny has been released by France to return to Arsenal for treatment on an achilles problem
Debuchy, Ospina na Ozil wote amewataja kuwa wanaendelea vizuri licha ya kusema kuwa hawatakuwemo kikosini kwa siku za hivi karibuni na matumaini ya kurejea kwao yakiwa baada ya michuano ya kimataifa kama ilivyo kwa Giroud.
 
 Mathieu Debuchy is also currently out of action after injuring himself against Manchester City

Post a Comment

 
Top