0
I'll take that: Manchester United players must hand over their mobile phones the night before a game

Wachezaji wa klabu ya Manchester United wanalazimika kukabidhi simu zao usiku mmoja kabla ya mechi yoyote watakayokua wanakwenda kucheza ikiwa hiyo ndio sheria mpya ya meneja mpya wa timu hiyo Mholanzi Louis van Gaal.

Sheria hiyo mpya imewekwa na Mholanzi huyo mara tu baada ya kuanza kuyatumikia madaraka yake mapya aliyoyatwaa kutoka kwa David Moyes.

Van Gaal hajaishia hapo kwani pia amewatahadharisha wachezaji wake kwa kuwaambia kuwa hatamjumuisha kikosini mchezaji yoyote yule atakayethubutu kuchelewa kwenye kifungua kinywa (Chai) ya asubuhi ya siku ya mchezo.

  Laying down the law: Van Gaal also drops any player who is late for breakfast on the morning of a game

Lakini sheria hizi mpya za meneja huyu zinaonekana kutokuzaa matunda kwani United bado inaendelea kuweweseka na jinamizi la matokeo mabovu kwani mpaka sasa katika michezo mitatu ya ligi iliyokwisha cheza hakuna hata mmoja ambao United wamepata matokea ya ushindi.

United wamefungwa kwenye mchezo wa ufunguzi wa ligi dhidi ya Swansea, lakini pia wametoka sare na Sunderland na Burnley bila ya kusahau kipigo cha mbwa mwizi walichokipata kutoka kwa MK Dons cha jumla ya magoli 4:0 kwenye michuano ya Capital One.
 
Van Gaal amekua hana taarifa zinazovutia sana kwenye masuala ya kiutawala kwani ziko taarifa zinazodai kuwa wakati yuko kwenye klabu ya Ajax wachezaji walikua wakilipishwa faini pindi walipokua wakichelewa kwaajili ya chai ya asubuhi na walilipishwa mara mbili zaidi walipochelewa kwa mara nyingine tena.

Training days: Van Gaal had £500,000 worth of cameras installed at United's Carrington training centre 

Wachezaji wote walitakiwa kuanza kula pamoja na inasemekana kuwa Van Gaal alikua akipendelea awasikie wachezaji hao wakizungumzia masuala ya mpira wa miguu.

Kwenye klabu ya Manchester United, Van Gaal ameamuru kuwa wachezaji wa kikosi cha kwanza na wale wa timu ya vijana wale chakula pamoja na chakula cha mchana ni lazima kiliwe saa saba kamili mchana bila kusahau kamera zenye thamani ya paundi 500,000 zilizofungwa kwenye uwanja wa mazoezi wa  Mancheste United (Carrington) zenye lengo la kuwaonesha wachezaji wanapotakiwa kuwepo wawapo uwanjani.

Post a Comment

 
Top