0
Suarez to Barcelona and the 10 most expensive transfers of the summer 

Dirisha la usajili la majira haya ya kiangazi kwa vilabu majira haya ya kiangazi limefungwa hapo jana usiku tukishuhudia miezi kadhaa ya kufuru ya matumizi yaliyokithili ya pesa kwa vilabu barani Ulaya.

 

Japokuwa rekodi ya uhamisho ghali zaidi duniani inashikiriwa na Gareth Bale ya uhamisho wa Euro milioni 100 alipohama kutoka Tottenham kwenda Real Madrid mwaka uliopita lakini mado suala la matumizi ya fedha na uvunjwaji wa rekodi mbalimbali linabakia palepale kwa vilabu kadhaa barani Ulaya.

Little bit hefty! United paid a club record £60million for Real Madrid midfielder Angel di Maria 

Wakati vilabu vikiendelea kusharehekea mapato makubwa kwenye matangazo na mauzo ya vifaa mbalimbali isivyo kawaida na vikienda kwenye duka kuu la ununuzi wa wachezaji ambalo ni michuano ya kombe la Dunia iliyofanyika kule nchini Brazil, Vilabu vinaonekana kuongeza ushindani pia kwenye matumizi ya mapato hayo makubwa wanayojikusanyia kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato.

Ufuatao ni usajili wa wachezaji kumi ambao wamenunuliwa kwa mahela mengi kwenye msimu huu wa manunuzi.

TOP 10 MOST EXPENSIVE TRANSFERS OF SUMMER 2014
No. Mchezaji Kutoka Kwenda Ada (Euro)
1 Luis Suarez Liverpool Barcelona 88m
2 James Rodriguez Monaco Real Madrid 80m
3 Angel Di Maria Real Madrid Manchester United 75m
4 David Luiz Chelsea Paris Saint-Germain 49.5m
5 Eliaquim Mangala Porto Manchester City 44.5m
6 Diego Costa Atletico Madrid Chelsea 44m
7 Alexis Sanchez Barcelona Arsenal 40m
8 Luke Shaw Southampton Manchester United 37.8m
9 Ander Herrera Athletic Bilbao Manchester United 36.5m
10 Cesc Fabregas Barcelona Chelsea 36m

Post a Comment

 
Top