0
Ruled out: The playmaker will miss the Champions League group stage clash against Arsenal on September 16
Kiungo wa klabu ya Borussia Dortmund, Nuri Sahin anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa kipindi kisichopungua miezi miwili kutokana na kufanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu hii leo. 

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 25 raia wa Uturuki aliyerejea kwenye klabu ya Dortmund mnamo mwaka 2013 mara baada ya kuwa na misimu mibovu akiwa na vilabu vya Liverpool na Real Madrid, alikokuwa anavitumikia kwa mkopo amefanyiwa upasuaji huo ambao inasemekana umefanyika kwa usalama.

Tough spell: Sahin endured a disappointing loan move to Anfield before re-signing at Borussia Dortmund

Katika taarifa hiyo iliyotolewa na dakatari wa klabu ya Borussia Dortmund Markus Braun amesema kuwa mchezaji huyo anatarajiwa kuwa nje kwa kipindi kisichopungua miezi miwili.

Dortmund, ambao wamemaliza katika nafasi ya pili ya ligi kuu ya nchini Ujeruman almaarufu kama Bundesliga kwenye msimu uliokwisha pia ni miongoni mwa timu zinazoshiriki michuano ya vilabu bingwa barani ulaya na kwa msimu huu imepangwa kwenye kundi D pamoja na vilabu vya Arsenal ya Uingereza, Galatasaray ya Uturuki na Anderlecht ya Uberigiji.

Sahin sasa anaungana na wachezaji wengine wa Dortmund kama Ilkay Guendogan, ambaye hajaitumikia klabu hiyo tangu mwaka uliopita, Jakub Blaszczykowski na Marcel Schmelzer katika orodha ya majeruhi wa klabu hiyo.

Post a Comment

 
Top