0

Meneja wa timu ya Borussia Dortmund Jurgen Klopp amekanusha taarifa zilizotolewa kwamba mchezaji wake Ilkay Gundogan aliyekua akisumbuliwa na majeruhi ya muda mrefu anatarajiwa kurejea siku ambayo timu yake ya Borussia Dortmund itakapomenyana dhidi ya Vfb Stuttgart.

Mara ya mwisho mchezaji huyu alikipiga kwenye mchezo ambao timu yake ya taifa ya Ujerumani ilikipiga dhidi ya Paraguay kwenye mchezo wa kirafiki uliofanyika siku ya August 2013.

Kiungo huyo anayesumbuliwa na maumivu ya mgongo ameendelea kujiuguza na maumivu hayo yanayomsibu na juzi kuliibuka taarifa kuwa mchezaji huyu yuko tayari sasa kurejea uwanjani siku timu hiyo itakapokipiga dhidi ya Stuttgart katika dimba la Signal-Iduna Park.

"Siku ambayo Ilkay Gundogan atarejea mchezoni litakua jambo kubwa kwa kila mmoja wetu ," Alisena Klopp.


Post a Comment

 
Top