0
Kocha Hans van Pluijm leo atakuwa na kazi moja ya kurudisha matumaini ya sana Yanga wakati atakapo kuongoza kikosi chake kucheza na MO Bejaia ya Algeria.

Hiyo ni mechi ya mzunguko wa tano katika kundi A la michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF.

Katika mchezo huo utakaopigwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam kikosi cha Yanga kinachoshikilia nafasi ya mwisho kwenye kundi hilo kitamkosa mshambuliaji wake mahiri Donald Ngoma mwenye kadi mbili za njano.


Mbali na Ngoma pia kocha Pluijm yupo katika hatihati ya kuwapoteza walinzi wake wawili wa kati Nadir Haroub 'Cannavaro' na Kelvini Yondani kutokana na majeruhi yanayo wakabili.

Nafasi hizo huenda zikazibwa na mabeki Vicent Bossou na Endrew Vicent ambao wameonekana kufanya vizuri kwenye mazoezi ya kuiandaa na mchezo huo wa kesho.

Pluijm amesema mchezo utakuwa mgumu kwasababu kila timu in a malengo na mbinu zao za mchezo waliojifundisha hivyo anauhakika na matoke .

Pluijm amesema maandalizi yao kuelea mchezo huo wa leo yamekamilika na kitu cha msingi kwao ni ushindi ili kufufua matumaini ya kucheza nusu fainali.


"Tunawakaribisha nyumbani Bejaia, lakini wajiandae kwa kupiga kwani ninaijua vizuri timu yao siyo nzuri wanacheza bila mpangilio na tulipokuwa kwao tuliwazidi kwa kumiliki mpira na kuwashambulia sana lakini walikuwa wakijiangusha na kupoteza muda," amesema Pluijm.

Mdachi huyo amesema kikosi chake cha kesho kinatarajiwa kuwa na mabadiliko kidogo hasa baada ya Ngoma kukosekana kwenye mchezo huo.

Kwaupaunde wao MO Bejaia, wametamba kuendelea kipigo kwa wawakilishi hao wa Tanzania kwasababu wananafasi nzuri nzuri ya kutinga nusu fainali.


Nahodha wa timu hiyo amesema kwa kuzingatia hilo ndiyo sababu wakaamua kuja mapema ili kuzoea hali ya hela lakini pia kupata muda wa kutosha wa kupumzika kabla ya mchezo huo ambao K wao wameupa umuhimu wa juu.

"Tunaiheshimu Yanga ni timu nzuri pamoja na kuwa nafasi ya mwisho ndiyo maana tumekuja mapema kuhakikisha tunashinda mchezo huo kwasababu tumejipanga vizuri na tunataka kucheza nusu fainali," amesema.

MO Bejaia ikishika nafasi ya tatu kwenye kundi A ikiwa na pointi 5 sawa na Medeama ya Ghana iliyopo nafasi ya pili lakini yenyewe ikiwa na wastani mzuri wa mabao.

Post a Comment

 
Top