

Gazeti la The Daily Star limeripoti kuwa United wamewapa Juve ofa ya paundi milioni 32 na kuchagua mmoja kati ya wachezaji hao wawili ili kukamilisha dili hilo la kumnasa kiungo huyo mchezeshaji.

Swali la msingi linalobakia vichwani mwa wadadisi wa mauala ya kisoka ni kuwa ni nani kati ya wanandinga hawa wawili atakayetolewa kama sadaka kwenda Juventus na pia klabu ya Juventus nayo itavutiwa na nani baina ya Chicharito na Danny Welbeck ili kumnasa Vidal

Ikumbukwe tayari meneja wa klabu ya Manchester United Louis Van Gaal alikwisha mwambia Welbeck kuwa milango iko wazi kwake kuondoka ndani ya Manchester United na kwenda kwenye klabu yoyote ambayo itaonesha nia ya kumuhitaji.
Post a Comment