
Brendan Rodgers akiwaangalia vijana wake mazoezini.
Sahau kuhusu mchezo wa
ngao ya jamii kwenye uwanja wa Wembley siku ya jumaamosi, Nchini marekani
kutakua na shughuli nzito ya kudhihilisha ubora wa vikosi baina ya Manchester
United na Livepool.
Mafahari hawa wawili
wanapokutana kitu pekee kinachotokea ni kila mmoja kutaka kumdhihilishia
mwenzake ni jinsi gani anatarajia kufanya au anafanya kwenye ligi na michuano
mbalimbali.
Kiungo wa Manchester
United Darren Fletcher amesema “ Ni mchezo kati ya Man Uited na Livepool.
Nafahamu kuwa nimchezo wa kujiandaa na msimuna ni mashindano ya kabla ya msimu
lakini Manchester United inapokutana na Liverpool siku zote huwa linakua jambo
kubwa.”
“Tunataka
kushinda mchezo huu kwakua tunatambua kuwa kushinda kila mchezo kunarejesha na
kuongeza ari ya timu na mashabiki”
United wana kumbukumbu
mbaya ya msimu uliokwisha kwani kwenye mchezo wao wa nyumbani dhidi ya Vijogoo
vya Anfield walipoteza mchezo kwa kukubali kichapo cha jumla ya goli 3:0.
Manchester imemwajiri miongoni mwa
makocha bora wa kiwango cha Dunia LvG na kwenye michezo yake ya mwanzoni mwa
msimu wamefanikiwa kuzifunga klabu za LA
Galaxy, AS Roma, Inter Milan na kuivurumisha Real Madrid jumla ya goli 3:1
kwenye uwanja wa Michigan ikishuhudiwa Young akifunga magoli mawili na lile
moja likiwekwa kimiani na Javier Hernandez (Chicharito).

Liverpool ilijihakikishia kucheza
fainali baada ya kupata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya AC Milan katika dimba la
Charlotte shukrani kwa magoli kotoka kwa Joe Allen naSuso,Ikishuhudiwa
Rickie Lambert akikosa mkwaju wa penati kwenye mchezo huo.
Ukiachilia mbali
upinzani mkubwa na wakihistori wa vilabu hivi lakini kuna kitu cha kukumbukwa
kuelekea mchezo huo kuhusiana na mameneja wa timu zote mbili ambapo meneja wa
klabu ya Livepool Brendan Rodgers atakutana uso kwa uso na bosi mpya wa klabu
ya Manchester Louis van Gaal mtu ambaye alimkataa kuwa mkurugenzi wa ufundi wa
klabu ya livepool miaka miwili iliyopita.
Louis van Gaal alifanya mazungumzo na
kukubaliana na Liverpool juu ya nafasi hiyo jambo ambalo Rodges alilikataa kwa
kusema ni bora afanye kazi na kundi la watu kulikoni kufanya kazi na mkurugenzi
wa ufundi.
“Ni jambo ambalo lilikuwepo hapo awali
kabla mimi sijaja hapa lakini mimi nahitaji kufanya kazi na kundi la watu
kuliko mkurugenzi wa ufundi.”
Post a Comment