0

Legend: Klose ends his career as Germany's all-time record scorer and second most-capped playerMshambuliaji wa timu ya taifa ya ujerumani, Miroslav Klose, ambaye aliweka rekodi ya kihistoria kwa kuwa mfungaji bora katika michuano ya kombe la duni mwaka 2014, baada ya kufunga mabao 6 peke yake, ametangaza kuustaafu

Mchezaji huyo wa klabu ya Lazio ya huko nchini Italy, mwenye umri wa miaka 36, ameeleza kwamba anastaafu baada ya ndoto yake ya utotoni kukamilika, ikiwa ni pamoja na ushindi wa timu ya taifa ya ujerumani nchini Brazil, ambayo ilitwaa kombe la dunia. Klose amesema michuano hiyo ya kombe la dunia iliyompa sifa hatoisahau maishani mwake.

 Perfect ending: Klose scored twice as Germany lifted the World Cup in Brazil this summer
Klose ni mchezaji wa pili wa Ujerumani kutangaza kustaafu katika ngazi ya kimataifa baada ya ushindi wa timu ya taifa ya Ujerumani nchini Brazil. Nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani, Philipp Lahm, mwenye umri wa miaka 30 alitangaza kustaafu siku 5 baada ya fainali kati ya Ujerumani na Argentina, jambo ambalo liliwaacha watu wengi vinywa wazi.

Klose ameweka rekodi ya kuwa mfungaji bora katika michuano ya kombe la dunia (mabao 16), ambayo ilikua inashikiliwa na Christian Ronaldo wa Brazil, ambaye alifunga mabao 15 kwenye guu lake katika michuano kama hiyo.

“Kwa kweli Miro, alionesha ujuzi wake na alitoa mchango mkubwa kwa timu ya taifa ya Ujerumani”, amesema Meneja wa timu ya taifa ya ujerumani Joachim Löw, akibaini kwamba anaheshimu uamzi wa Miroslav na mchango aliotoa kwa timu ya taifa.
 On target: Klose breaks the all-time World Cup scoring record against hosts Brazil
"Katika masuala ya soka na utu, tutamkumbuka Miroslov”, amemalizia Löw, akinukuliwa kwenye mtandao wa shirikisho la soka la Ujerumani (DFB).

Rais wa shirikisho la soka nchini Ujerumani, Wolfgang Niersbach, amebaini kwamba Klose hakua tu mchezaji tofauti na wengine, alikua pia mtu wa kuigwa.

“Kufuatia mabao 71 aliyofunga akiichezea timu ya taifa ya ujerumani na mabao 16 aliyofunga katika michuano ya kombe la dunia, ameweka rekodi mbili muhimu ambayo itampelekea kupata na fasi ya heshima katika kitabu cha kihistoria", amesema Niersbach.

Respect: Klose shakes hands with Germany boss Joachim Low during a quarter-final clash with France
Ifuatayo ni orodha ya mabao yote 16 ya mshambuliaji huyo  kwenye michuano mbalimbali ya Dunia.

1, 2, 3: Germany 8-0 Saudi Arabia, hatua ya makundi kombe la Dunia-2002
4: Germany 1-1 Republic of Ireland, hatua ya makundi kombe la Dunia-2002
5: Cameroon 0-2 Germany, hatua ya makundi kombe la Dunia-2002
6, 7: Germany 4-2 Costa Rica, hatua ya makundi kombe la Dunia-2006
8, 9: Ecuador 0-3 Germany, hatua ya makundi kombe la Dunia-2006
10: Germany 1-1 Argentina nusu fainali kombe la Dunia-2002
11: Germany 4-0 Australia, hatua ya makundi kombe la dunia-2010
12: Germany 4-1 England, hatua ya 16 bora kombe la dunia-2010
13, 14: Argentina 0-4 Germany, nusu fainali kombe la Dunia-2010
15: Germany 2-2 Ghana, hatua ya makundi kombe la Dunia-2014
16: Brazil 1-7 Germany, nusu fainalikombe la dunia-2014


Post a Comment

 
Top