0
MSHAMBULIAJI wa Stand United Elias Maguri amesema anaweza kujiunga na timu yoyote, lakini siyo Simba ambayo ilimdhalilisha kwa kusema hana kiwango cha kuichezea timu hiyo.

Maguri amesema hataki kurejea Simba na zaidi anafikiria kwenda kucheza soka nje ya Tanzania endapo atashindwa kusajiliwa na timu nyingine za ndani.

“Ukweli siwezi tena kurudi Simba kutokana na tulivyoachana nipo tayari kuchezea timu nyingine yoyote laki siyo wao na kwa sasa nina mtu ambaye ananisimamia, huyo ndiye anazungumzia mambo yangu,”amesema.

Maguri ndiye anaongoza kwa mabao katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara hivi akiwa amefunga mabao tisa katika mechi 10 alizocheza Stand United ikiwa ni muda mfupi tangu alipoachwa na Simba.

Post a Comment

 
Top