
Mshambuliaji wa Wilfried Bony amesaini mkataba wa miaka minne unusu kuichezea timu Manchester City wenye thamani ya paundi 28 milion.

Bony amekubali mkataba huu na atavaa jezi namba 14 iliyokua ikitumiwa na nyota na Javi Garcia.

Baada kusajiliwa na City Bony ameelezea "Ni heshima kubwa kuwa hapa na ni changamoto kwangu".

Mchezaji
huyo mwenye miaka 26 alitua ligi ya England mwaka 2013 akijiunga na
klabu ya Swansea akitokea Vitesse Arnhem ya Uholanzi kwa ada ya uhamisho
ya paundi 12 milioni na kuwa moja kati ya wafungaji bora katika ligi kuu.

Kwa uhamisho huu unamfanya Bony kuwa mmoja kati ya wachezaji wa Afrika wanaolipwa pesa nyingi duniani katika mchezo wa soka.
Post a Comment