
Mshambuliaji huyo anayelipwa mshahara wa paundi 346,000 kwa wiki hakutaka hata kuutazama mchezo huo ambao timu yake iliambulia kichapo cha goli 1:0 kwani aliondoka na usafiri wake binafsi kabla hata ya mchezo kuanza.

Meneja wa klabu ya Manchester United Louis van Gaal
alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusiana na sababu za kimsingi za kumuacha mshambuliaji huyo alisema kuwa alifanya hivyo ili kuwapa nafasi ya kuwepo kikosini walinzi Jonny Evans, Paddy McNair na Tyler Blackett na mshambuliaji James
Wilson.
Falcao, ameanzishwa kwenye michezo takribani saba tu tangu alipotua Ot na kufanikiwa kuwafungia mashetani wekundu hao jumla ya magoli mawili muhimu ambayo yameisaidia klabu hiyo kupata alama muhimu kwenye michezo dhidi ya Stoke na Aston Villa.
Post a Comment