
Tuzo hizo zinazotarajiwa kutolewa mnamo January 8, mwaka 2015 zinaonekana kuwa na ushindani mkubwa kutokana na aina ya wachezaji waliojumuishwa kwenye shindano hilo na sifa zao.Jumla ya wachezaji 25 wametajwa kuwania tuzo hiyo akiwemo Ahmed Musa ambaye kwa sasa anafanya vyema akiwa na klabu yake ya CSKA Moscow ya nchini Urusi ambaye aliiongoza vyema timu yake hiyo kuwafumua Manchester City kwenye mchezo wa makundi ya michuano ya UEFA Champions League,Lakini yumo pia na Mehdi Benatia mchezaji pekee wa kiafrika aliyenufaika na uhamisho wake wa kujiunga na klabu ya Bayern Munich, Lakini pia katika orodha hiyo wamo pia wachezaji maarufu wanaotoka katika bara hili kama vile; Emmanuel Adebayor, Stephane Mbia,
Islam Slimani na Asamoah Gyan.
Washindi waliopita wa tuzo za BBC za mchezaji bora wa Afrika:
2013 -
Yaya Toure
(Manchester City & Ivory Coast)
2012 -
Chris Katongo
(Henan Construction & Zambia)
2011 -
Andre Ayew
(Marseille & Ghana)
2010 -
Asamoah Gyan
(Sunderland & Ghana)
2009 -
Didier Drogba
(Chelsea & Ivory Coast)
2008 -
Mohamed Aboutrika
(Al Ahly & Egypt)
2007 -
Emmanuel Adebayor
(Arsenal & Togo)
2006 -
Michael Essien
(Chelsea & Ghana)
2005 -
Mohamed Barakat
(Al Ahly & Egypt)
2004 -
Jay-Jay Okocha
(Bolton & Nigeria)
2003 -
Jay-Jay Okocha
(Bolton & Nigeria)
2002 -
El Hadji Diouf
(Liverpool & Senegal)
2001 -
Sammy Kuffour
(Bayern Munich & Ghana)
2000 -
Patrick Mboma
(Parma & Cameroon)
Post a Comment