
HATIMAYE timu ya Coastal Union imefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa
Stand United Mnigeria Abasalim Chidiebele kwa kumpa mkataba wa mwaka
mmoja.
Chidiebele aliyeshika nafasi ya tatu kwa ufungaji kwenye ligi ya msimu uliopita amethibitisha hilo kwa kusema ametua Coastal Union baada ya kuvutiwa kwa ofa ambayo wamempa na
kuahidi atahakikisha anajituma ili azidi kufanya vizuri zaidi ya
ilivyokuwa Stand.
Meneja wa Coastal Union, Akida Machai amesema kwa muda mrefu walikuwa
wakimfuatilia mshambuliaji huyo na baada ya kumnasa sasa wanauhakika
watafanya vizuri msimu ujao na kubigania ubingwa wa Tanzania bara.
Coastal Union ipo katika harakati za kukijenga upya kikosi chake
baada ya kuvunja mikataba ya idadi kubwa ya wachezaji wake iliyokuwa nao
msimu uliopita kwa matatizo mbalimbali.
Post a Comment