0
Match Preview: Yanga - Coastal Union, Mabingwa kuanza na mwendo ule ule

KOCHA Hans van der Pluijm, leo Jumapili ataingia majaribuni ya kutetea ubingwa wake wa Ligi ya Vodacom Tanzania bara wakati itakapokuwa nyumbani uwanja wa taifa Dar es Salaam kuwaalika Coastal Union ya Tanga.

Huo utakuwa ni mchezo pekee kwa siku ya leo ikiwa ni siku ya pili tangu kuanza kwa msimu mpya wa Ligi hiyo inayoshirikisha timu 16.

Yanga inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na rekodi nzuri mbele ya Coastal Union,ambayo msimu uliopita iliweza kushinda mechi zote mbili ikiwemo kupata ushindi mnono wa mabao 8-0 katika mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja huo wa taifa.

Kinachompa matumaini ya kushinda mchezo huo kocha Pluijm, wa Yanga ni usajili walioufanya kwa kuongeza wachezaji wapya saba kwenye kikosi chake wakiwemo nyota wakimataia Donald Ngoma na Thaban Kamusoko wa Zambabwe na wazawa Malimi Busungu,Mateo Simon ,Haji Mwinyi na Vicent Bossou raia wa Togo.

Kuwepo kwa nyota hao kunaonekana kukiimarisha zaidi kikosi cha Yanga ambacho katika mchezo wa leo kitawakosa mrisho Ngassa na Kpah Sherman ambao wamesajiliwa na timu za Afrika Kusini.

Katika mchezo wa leo niwazi Pluijm, atataka kuanza kwa kutoa onyo kwa kupata ushindi mnono ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kuongoza ligi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa msimu huu.

Wachezaji kama Ngoma,Kamusoko wanatarajia kuanza kikosi cha kwanza huku kipa Ally Mustapha ‘Barthez’ akianzia golini huku akilindwa na mabeki Nadir Haroub na Kelvini Yondani.

Beki wa kushoto Haji Mwinyi, anatarajiwa kuwepo kwenye kikosi cha Pluijm, kwa ajili ya kusaidia mashambulizi ya upande wa kushoto kwa kupiga krosi ambazo zitakuwa zikiwakuta akina Ngoma na Amissi Tambwe, ambao kazi yao kubwa itakuwa ni kihakikisha nyavu zinacheza.

Pluijm amesema, aahitaji kupata ushindi wa mabao 3 kwenda mbele kutokana na uimara wa kikosi chake na ukali wa safu yake ya ushambuliaji.

“Nimchezo mwepesi ambao hauniumizi kichwa kama kocha kwasababu ya ubora wa kikosi changu na mapungufu waliyokuwa nayo wapinzani wetu Coastal Union,”amesema Pluijm.

Kwaupande wake kocha wa Coastal Union Jackson Mayanja, ametamba kuwa wapo Dar es Salaam kuhakikisha wanapata ushindi na hawaihofii Yanga kwasababu kwake ni timu kama zilivyo timu nyingine.
Mayanja mabaye msimu uliopita alikuwa akiifundisha Kagera Sugar amesema anazijua vyema mbinu za kocha Pluijm, wa Yanga na mara zote amekuwa akiifunga Yanga wakati akifundisha Kagera.

“Tunacheza na Yanga nikweli timu kubwa na tunawaheshimu kwakua ni mabingwa lakini tumejipanga kuwafunga wakiwa nyumbani,”amesema Mayanja.

Mayanja kwa kiasi kikubwa amekibadilisha kikosi cha Coastal kwa kusajili sura nyingi mpya akiwemo Chidiabele Abasalim raia wa Nigeria ambaye alishika nafasi ya tatu kwenye orodha ya wafungaji msimu uliopita.

Pia kwenye kikosi hicho yupo Twaha Shekuhe ‘Messi’ aliyekuwa akiichezea Simba mchanganyiko huo ndiyo unaotarajiwa kusababisha ushindani mkali kwenye mchezo huo wa leo.
Chanzo; Goal.com

Post a Comment

 
Top